Uefa Champions League Barcelona 5-1 Panathinaikos Benfica 2-0 Hapoel Tel-Aviv Bursaspor 0-4 Valencia FC Copenhagen 1-0 Rubin Kazan FC Twente 2-2 Inter Milan Lyon 1-0 Schalke 04 Man Utd 0-0 Rangers Werder Bremen 2-2 Tottenham
Kiungo wa pembeni wa Klabu ya Manchester United Antonio Valencia huenda akawa nje ya Uwanja kwa msimu mzima baada ya kuumia katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya Rangers kwenye Dimba la Old Trafford!! Kocha Mkuu wa Man Utd amenukuliwa akisema mchezaji wake amepata maumivu mabaya sana ya kifundo cha mguu na huenda akawa nje kwa muda mrefu!!!
Hizi ni shamra shamra za Miaka 48 ya Uhuru ambazo zimefanyika katika Uga wa Uhuru. Miaka 48 iliyopita hapa nchipo Waingereza waliposali amri na kutuacha tuwe huru. Amiri Jeshi Mkuu Rais Dr Jakaya Mrisho Kikwete akiingia Uwanja pamoja na kukagua gwaride. Picha kwa Hisani ya Uncle Michuzi.
Hakika maadhimisho ya miaka 48 ya Uhuru wa Tanganyika yamekwenda vizuri. Lakini watu wanaendelea kumkumbuka Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakiamini bila ya yeye nchi isingekuwa hapo. Kwa kuwa yeye akishirikiana na wazalendo wengine walifanikisha upatikanaji wa Uhuru. Hurreee Tanganyika!!!